Wednesday, January 20, 2010

Kiongozi Muadhamu: Viongozi wa jamii wanapaswa kuweka wazi misimamo yao mbele ya adui

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya kiislamu ya Iran Ayatullah Ali Khamenei leo amehutubia hadhara kubwa ya maafisa wa Baraza la Uratibu la Jumuiya ya Ulinganiaji wa Kiislamu nchini na viongozi wa kamati za Alfajiri 10 na sherehe za Mapinduzi ya Kiislamu akisema kuwa wadhifa wa wananchi wote hususan watu wenye nafasi za juu za kijamii katika kipindi cha fitina na mazingira ya kutatanisha ni kuonyesha msimamo wa wazi na kujiepusha na maneno na misimamo isiyoeleweka vyema. Ameongeza kuwa maadui daima wanapinga suala la kuwepo mazingira ya uwazi kwani wanaweza tu kufikia malengo yao katika mazingira ya kutatanisha na yenye fitina. Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, katika kipindi cha sasa mirengo na makundi yote ya kisiasa ndani ya mfumo wa Kiislamu hapa nchini yanapaswa kuweka wazi misimamo na mipaka inayowatenganisha na maadui, na kwamba suala hilo ni wajibu zaidi kwa watu wenye ushawishi na taathira kubwa katika jamii. Si sahihi kuwa na msimamo au kutoa maneno yasiyokuwa ya wazi wakati viongozi wa ubeberu na dhulma na wavamizi wa nchi za Kiislamu wanapoingia katika medani na kudhihirisha misimamo yao. Ayatullah Khamenei amesema, wakati baadhi ya watu wanapokana Uislamu katika maneno na kupinga Jamhuri ya Kiislamu kivitendo kisha wakahoji uhalali wa uchaguzi wa Rais hapa nchini katika mazingira ya fitina na yaliyojaa vumbi, inatarajiwa kwamba watu wenye nafasi za juu katika jamii wanapaswa kudhihirisha wazi misimamo yao.Amesema: "uwazi ni adui wa maadui na kuzusha anga ya fitina na vumbi ni kumsaidia adui". Amesisitiza kuwa hicho ni kigezo na mizani ya utendaji kazi watu na makundi yote hususan tabaka la watu wenye nafasi za juu na ushawishi mkubwa katika jamii. Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezungumzia njama mbalimbali zilizofanywa dhidi Mapinduzi ya Kiislamu katika kipindi cha miaka 30 iliyopita na akasema: "Taifa la Iran limepita katika misukosuko na vipindi vigumu mno kwa rehema yake Mwenyezi Mungu na litavuka mashaka kama hayo. Amesema kuwa maana ya mahudhurio hayo makubwa ya kila mwaka ni kuwa Mapinduzi ya Kiislamu na mfumo wake yanategemea wananchi na imani yao na hii ndiyo sababu kuu ya kushindwa kwa maadui katika njama zao za kuteteresha mfumo wa Kiislamu nchini Iran.Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa mti madhubuti wa Mapinduzi ya Kiislamu utaendelea kutoa matunda zaidi licha ya njama zote za maadui.

No comments:

Post a Comment